Ijumaa, 28 Aprili 2017

UHALISIA WA MAISHA YA NDOA.
SEHEMU YA KWANZA
kabla hatuaja anagalia yaliyo katika ndoa Tutazame Maneno haya ya Daudi, Zaburi 127:1-2 "Bwana asipoijenga nyumba Waijengao wafanya kazi bure. Bwana asipoulinda mji Yeye aulindaye akesha bure.
Kwa wana ndoa na Wale wasio wana ndoa soma hii yaweza kusaidia
SEHEMU YA KWANZA.
UTANGULIZI:
Kwa kuanza tutazama haya maeneo kadhaa amabayo yanahusu ndoa nyingi za watu wenye maisha amabayo ni mfano mbele za watu lakini ndani ya ndoa yanaweza yakawa ni sehemu ya maisha yao na hawawezi mwambia mwingine au hata wakisema huwa hayana majibu na suluhu.
1. Wengi huwa na maswali kuhusu ndoa na wachache wanayo majibu ya maswali hayo. na wengine wanaishi katika ndoa lakini hawana majibu ya maswali ya yale yanayo endelea katika ndoa zao. hivyo huishi kwasababu kwa kuwa washafunga ndoa na hawana namna nyingine tena ya kubadili huo uhalisia.
2. Wengi huamini kuwa wamekosea au wamewahi kuoa na kuolewa na huyo mtu, na wengine ambao hawaja ingia katika ndoa hutazama watu vile wanaishi na kualinganisha na maisha wanayo tarajia katika ndoa na kuwafanya waogope kuingia katika ndoa au kuingia wakiwa na mashaka
3. Wengi husema mwenzi wake kabadilika mara baada ya kuingia katika ndoa na hajui kwanini. kabla ya kuingia katika ndoa alitamani awe na ndoa ya mfano, lakini kakutana na ndoa iliyo mjeruhi na kuendelea kumuumiza na kumfanya atake ndoa mpya "kitu kisicho wezekana"
4. Kabla ya kuingia kwenye ndoa mwenzi wako alikuwa anapendeza sana lakini baada ya kuolewa/kuoa hapendezi tena kama mwanzo, na hii imetambulika kwako na kwake imesabisha kupoteza uhuru wa kutoka faragha pamoja, au imekuwa sehemu ya wengine kuogopa kuoa na kuolewa.
5. Kabla ya kuingia kwenye ndoa mwenzi wako alikuwa anajari sana, anajitoa kwaajili yako, alikuwa anakushirikisha yote, alikuwa anakupa uhuru wote, alikuwa anakufanya mtu muhimu sana kwake lakini baada ya kuoa ua kuolewa mwenzi wako hana habari na wewe. hana muda wa kupanga na kujadili nawe. ndoto za wakati wa uchumba zimekufa, utekelezaji na utendaji wa mambo mema haupo tena, tabia usizo zijua ndoa zimetawala maisha yake.
NB: MASWALI YA KUJIULIZA:
i) KWANINI HAYA HUTOKEA
ii) JE MTU HUBADILIKA
III) kWANINI YATOKEE BAADA YA KUOA AU KUOLEWA
IV) JE NI KWELI UMEKOSEA KUOA AU KUOLEWA
V) JE NI KWELI MWENZI WAKO AKUPENDI
Tukutane sehemu ya Pili tuendelee kutazama ukweli katika ndoa!!
++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
Ndoa ni mwili moja: Ikiwa ni mwili mmoja unapaswa kuulisha, kuujali, na kuutunza kama vile unavyo fanya kwako mwenyewe, unapaswa kufanya zaidi kwa mwenzi wako.
By (THE VOICE OF VICTORY)

Jumanne, 1 Oktoba 2013

KWA UNAYE TAKA KUJIUNGA NA UMOJA HUU KIOFISI.

UNAYE HITAJI KUJIUNGA NA UMOJA WA VIJANA WA KIKRISTO TANZANIA, TUNAOMBA UTUMIE EMAIL YAKO KUPITIA BLOG HII,AU WALL NA PAGE YA Umoja Wa Vijana wa kikristo Tanzania, Na Email Yetu jesus4youth@gmail.com. Ili tukutumie fomu ya kujinga na Katiba ya Umoja huu.

Unaweza kutuma kwa Email yako Au facebook Msg au comment chagua njia iliyo sahihi, rahisi na salama kwako.

"Tunakupenda Barikiwa"

Jumapili, 22 Septemba 2013

RASIMU YA KATIBA YA USHIRIKA WA VIJANA WA KIKRISTO TANZANIA

TUNAPENDA KUSHIRIKIANA NAWE KATIKA UNDISHI WA KATIBA YA USHIRIKA WA VIJANA WA KIKRISTO TANZANIA.


  • WAPENDWA TUNAOMBA MPITIE RASIMU HII YA KATIBA ILIYOTUMWA KWA WACHUNGAJI KISHA KOSOA,TOA MAONI,ONGEZA KITU AU SHAURI JAMBO AU ULIZA. KISHA TUMA KWENYE EMAIL HII jesus4youth@gmail.com



RASIMU YA KATIBA YA USHIRIKA WA VIJANA WA KIKRISTO TANZANIA

1. SEHEMU YA KWANZA

UTANGULIZI
Ibala 1. JINA LA KIKUNDI.Kikundi hiki kitajulkana kama CHRISTIAN YOUTH FELLOWSHIP IN TANZANIA (CYFT) kwa kiswahili USHIRIKA WA VIJANA WA KIKRISTO TANZANIA 
S .L.P. 245, Mbeya.
 Mahali Tulipo MBEYA.

Dira.
Dira ya Ushirika wa vijana wa kikristo Tanzania  “Ni kuunganisha vijana wa kikristo Tanzania kuhakikisha wanamtumikia Mungu kwa pamoja bila kujari udhehebu wao.”kwa kutambua umuhimu wa kumtumikia Mungu tukiwa bado vijana na kuondoa mipaka ya madhehebu tukana ni vema tukaungana ili kuujenga Mwili wa Kristo katika maeneo yetu tunayo ishi,fanya kazi, soma na Kuabudu. Hivyo tukaona vema kuanzisha Ushirika wa Vijana Wa Kikristo Tanzania kwa ngazi ya Taifa, Mikoa na Wilaya.

Dhima Ni kuunganisha vijana wa kikristo TANZANIA ili tumtumikie MUNGU.Lengo ni  kuhubiri neno la Mungu katika kila eneo kwa njia zote yaani Uimbaji,uinjilisti,uwalimu,unabii,uchungaji na utume.kuandaa mikutano ya injili,semina za ndani na nje,makongamano ya kusifu,kuabudu na maombi. Kutembeleana,kushauriana,kusaidiana,kubadilishana mawazo,ujuzi na ufahamu kuhusu maisha ya vijana ili kufanikiwa kiroho na mwili.Kusaidiana katika changamoto za ujana,Hasa katika uchumi,Mahusiano,Ndoa,Huduma,Elimu,jamii na kazi za kila siku





SEHEMU YA PILI.
Ibala 2. IMANI

a)      Tukiwa kama Ushirika Wa Vijana wa Kikristo Tanzania tunamkubari YESU KRITO kuwa ni BWANA na MWOKOZI wa watu wote.
b)      Tunayaamini maandiko matakatifu yaani BIBLIA kuwa ni NENO la Mungu nalo ni kweli na takatifu.
c)      Tunaamini kuwa YESU KRISTO alikufa na akafufuka na kuwa ROHO MTAKATIFU anafanya kazi kati yetu na MUNGU baba ndiye muumba wa mbingu na nchi.
d)     Hatu amini katika Dhehebu,dini au Mtu binafsi.

SEHEMU YA TATU

Ibala 3:MADHUMUNI YA USHIRIKA.
1.Kuhubiri injili ili watu wampokee YESU KRISTO kuwa BWANA naMWOKOZI wa maisha yao na kwasaidia vijana waishi kwa kufuata Misingi ya Kristo huku wakishuhudia na kutangaza/kuhubiri habari njema na kumtumikia MUNGU katika nchi yao na ulimwengu wote.

2.Madhumuni Mahususii
(i)        Kuandaa semina,kambi za maombi na mikesha ya kusifu na kuabudu kwa ajili ya Taifa la Tanzania. 
(ii)      Kuhamasisha vijana wa kikristo bila kujali udhehebu wao kumtumikia Mungu katika maeneo yao na Tanzania kwa ujumla. 
(iii)     Kufungua miradi itakayo endeshwa na ushirika wa vjana wa kikristo Tanzania.
(iv)    Katafuta na kutoa fulsa za ajira kwa vijana bila kujali dhehebu dini au kabila 
(v)      Kutembeleana,kushauriana,kusaidiana,kubadilishana mawazo,ujuzi na ufahamu kuhusu maisha ya vijana ili kufanikiwa kiroho na mwili.Kusaidiana katika changamoto za ujana,Hasa katika uchumi,Mahusiano,Ndoa,Huduma,Elimu,jamii na kazi za kila siku.


SEHEMU YA NNE
 Ibala4:UANACHAMA NA MASHARITI.
 Kijana kutoka katika kanisa lolote Tanzania linalotambulika kiserikali na kijami

(i)     Jinsi ya kujiunga na Umoja.
a)            Atajaza fomu ya maombi ya uwana chama wa kudumu kwa Tawi,Wiaya na Mkoa Husika itakayo patikana Katika ofisi na tovuti/blog  au mwakilishi wa umoja huu.
b)            Atajadiliwa na kukubaliwa na wanachama wa ngazi husika
c)            Atapewa taarifa za kuwa Mwanachama na Viongozi wa ngazi husika.

(ii)   Mashariti ya Uwana chama.
(i)              Atakubaliana na katiba ya Ushirika Wa Vijana Wa Kikristo Tanzania (UVIKITA)
(ii)            Baada ya kujiunga atatakiwa kulipia ada kitambulisho cha mwanachama kila mwaka kwa ngazi husika.
(iii)          Atashiriki katika shughuli za umoja na kutoa michango Muhimu pale inapotakiwa
(iv)          Awe ni mtanzania mwenye akili timamu na mwenye umri usio pungua miaka 18
(v)            Awe mwaminifu kwa Mungu na mwenye utayari wa kufanya kazi ya Mungu. 

Ibala5: HAKI ZA MWANACHAMA
(i)              Mshirika atakuwa na haki sawa katika umoja bila kujali jinsia yake. 
(ii)            Anayo haki ya kuchangia mawazo na ya kupata taarifa mbalimbali zinazomuhusu umoja 
(iii)          Kila mwanachama anayo haki ya kutumia kipaji chake kubuni, kuunda na kutengeneza kitu chochote anacho fikiria kwa kuwashirikisha na kukubaliana na viongozi wa umoja.
(iv)          Mwana chma ana haki ya kukosoa au kukosolewa au kutoa maoni ya kuimarisha umoja
(v)             Ana haki ya kushitaki/kushitakiwa kwenye vyombo vya sheria 
(vi)          Haki ya kuajiriwa na Ushirika huu na afuate mkataba wa kazi apewe muda na ausome na kuridhia.

   Ibala6: KUKOMA AU MWISHO WA MWANACHAMA
(i)              Mwanachama atapoteza uwana chama endapo atakiuka Katiba ya UVIKITA
(ii)            Kutopoteza ushuhuda mzuri wa Kikristo kwa umoja huu na jamii inayo mzunguka
(iii)          Kukiuka,kuupuuza au kufanya jambo lililo nje na lengo au makubalino ya umoja kwa manufaa bainafsi.


  SEHEMU YA TANO
  UONGOZI
  Ibala 7:Viongozi
     Muundo wa ungozi katika Ushirika huu unanzia ngazi ya Tawi, Wilaya, Mkoa na Taifa.
a)      Muundo wa ungozi kwa ngazi ya Tawi, Wilaya na Mkoa utakuwa:-
(i)        Mwenyekiti
(ii)      Makamo mwenyekiti
(iii)    Katibu
(iv)    Makamo katibu
(v)      Mhazini
(vi)    Mwenyekiti wa Maombi

b)      Muundo wa uongozi kwa ngazi ya Taifa utakuwa:-
(i)        Mratibu mkuu
(ii)      Katibu mkuu
(iii)    Mhazini
(iv)    Mwenyekiti wa Maombi
(v)      Makamo mwenykiti wa maombi

  Ibala8: SIFA ZA VIONGOZI
  Viongozi wa ushirika huu wanatakiwa wawe na sifa zifuatazo:-
a)      Awe mwaminifu kwa Mungu.
b)      Awe anafuata katiba ya ushirika.
c)       Awe mwenye kujituma, kujitolea, mpenda kazi na mwenye ushirikiano na wengine bila kujali jinsia
d)     Awe mwaminifu na muwazi kwa wengine.
e)      Awe mwenye unyenyekevu (utii) asiye tanguliza maslahi binafsi
f)       Awe anayetoka kwenye kanisa la kikristo linalo tambulika kiserikali na kijamii na lenye ushuhuda mzuri.
g)      Awe anatambulika kwa uongozi wa Kanisa lake na mwenye kushirikiana vema.




Ibala 9: WAJIBU WAVIONGOZI
KITAIFA, MKOA, WILAYA NA TAWI
1)      Mratibu kuu,Mwenyekiti wa Tawi, Wilaya, Mkoa.
(i)     Kusimamia na kuaratibu shughuli zote ushirika kwa ngazi husika
(ii)   Kuitisha vikao vya kamati kuu kwa kupitia katibu.
(iii) Mwendeshaji na msimamizi wa matukio yote kwa ngazi husika
(iv) Mshauri katika shughuli za Mikoa (Mratibu mkuu Taifa)
(v)   Kuhusika katika maswala yote fendha kwa kutia sahihi
(vi) Kubeba dhamana ya mali zote za ushirika.

2)      Katibu wa Taifa, Mkoa, Wilaya na Tawi
(i)     Ndiye mtendaji mkuu na mfuatiliaji wa shughuli zote kwa ngazi husika
(ii)   Kukusanya na kutunza taarifa na takwimu zotekitaifa
(iii) Kupanga na kutoa taaria za matukio ya kitaifa ikiwa na vikao.
(iv) Mwandishi wa vikao vyote vya ushuka na kusoma makubaliano.
(v)   Kutuma na kupoke barua zote na kuzifikisha mahali husika
(vi) Kubeba dhamana ya mali zote za ushirika

3)      Mtunza Hazina
(i)     Kupokea na kutoa fedha kwa shughuli zote za ushirika
(ii)   Kutunza mali na kusimamia miradi yote ya ushirika(kubeba dhamana)
(iii) Kupeleka fedha Benki na kutunza kumbukumbu za kifadha kwa ushirila
(iv) Kutoa stakabadhi kwa kila fedha ya malipo na kutunza vitabu vya risiti
(v)   Kutia sahihi Benki wakati wa kuweka au kutoa fedha

4)      Mwenyekiti wa Maombi
(i)     Kundaa shughuli zote za kiroho na maombi kwa ngazi husika
(ii)   Kuhakikisha injili neon la Mungu linafika maeneo yote
(iii) Kulea na kusimamia maisha ya kiroho ya kanisa kwa ngazi husika
(iv) Kushiriki katika matukio ya umoja kwa ngazi husika
(v)   Kubeba dhamana ya mali zote za ushirika kwa ngazi husika.






SEHEMU YA  SITA
MUUNDO
Ibala10:Kamati kuu ya Tawi
(i)                 Kamati kuu ya tawi inahushisha:-
Mwenyekiti. Makamu mwenykiti. Katibu. Mtunza hazina. Mwenykiti wa maombi. Makamu mwenyekiti wa maombi na mshauri wa tawi.

(ii) Wajibu wa kamati hii utakuwa:
a)      Kusimamia shughuli zote za tawi.
b)      Kuandaa agenda na kusimamia vikao vya tawi
c)      Kuandaa na kutoa taarifa zinazohusu shughuli zote za uendeshaji wa tawi kwa halmashauri kuu ya tawi na kamati kuu ya wilaya.
d)     Kuaandaa vikao visivyopungua vinne kwa mwaka kama kamati kuu.
e)      Kuandaa mikutano ya halmashauri kuu ya tawi isiyo pungua mitatu kwa mwaka.
f)       Kushiriki na kuhusika kwenye matukio ya wilaya,mkoa na Taifa kwa ujumla
g)      Kuandaa na kufanya matukio kwa wilaya yao.
h)      Kuhudhuria na kushiriki vikao vya halmashauri kuu ya wilaya yao
i)         Kujadili mwenendo mzima wa umoja na kupanga mikakati ya kuiendesha.
j)        Kupanga bajeti ya umoja na kuiwasilisha kwenye Halmashauri kuu.
k)       Kuibua na kupanga miradi mbalimbali ya umoja na kuijadili kwenye halmashauri kuu.
l)         Kupanga mipango ya muda mfupi na muda mrefu kwa ajili ya maendeleo ya umoja
m)    Kupitia maombi ya wanachama na kuyajibu na baadaye kuyawasilisha kwenye halmashauri kuu


Ibala 11:Kamati kuu ya Wilaya
(i)                 Kamat kuui ya wilaya inahusisha:-
Mwenyekiti. Makamu mwenykiti. Katibu. Mtunza hazina. Mwenykiti wa maombi. Makamu mwenyekiti wa maombi na mshauri wa wilaya

(ii)               Wajibu wa kamati hii utakuwa:-
a)      Kusimamia shughuli zote za wilaya.
b)      Kuandaa agenda na kusimamia vikao vya wilaya
c)      Kuandaa na kutoa taarifa zinazohusu shughuli zote za uendeshaji wa wilaya kwa halmashauri kuu ya wilaya na kamati kuu ya mkoa.
d)     Kuaandaa vikao visivyopungua vinne kwa mwaka kama kamati kuu.
e)      Kuandaa mikutano ya halmashauri kuu ya wilaya isiyo pungua miwili kwa mwaka.
f)       Kufanya ziara za mara kwa mara katika matawi yao
g)      Kushiriki na kuhusika kwenye matukio ya mkoa na Taifa kwa ujumla
h)      Kuhudhuria na kushiriki vikao vya halmashauri kuu ya Mkoa wao.
i)        Kujadili mwenendo mzima wa umoja na kupanga mikakati ya kuiendesha.
j)        Kupanga bajeti ya umoja na kuiwasilisha kwenye Halmashauri kuu.
k)       Kuibua na kupanga miradi mbalimbali ya umoja na kuijadili kwenye halmashauri kuu.
l)         Kupanga mipango ya muda mfupi na muda mrefu kwa ajili ya maendeleo ya umoja
m)    Kupitia maombi ya wanachama na kuyajibu na baadaye kuyawasilisha kwenye halmashauri kuu



Ibala12 :Kamati ya mkoa.
(i)                 Kamati kuu ya mkoa inahusisha:-
Mwenyekiti. Makamu mwenykiti. Katibu. Mtunza hazina. Mwenykiti wa maombi. Makamu mwenyekiti wa maombi na mshauri wa mkoa.

(ii)               Wajibu wa kamati hii utakuwa:-
a)      Kusimamia shughuli zote za wilaya,mkoa na Taifa.
b)      Kuandaa agenda na kusimamia vikao vyote vya mkoa
c)      Kuandaa na kutoa taarifa zinazohusu shughuli zote za uendeshaji wa mkoa kwa halmashauri kuu ya mkoa na kamati kuu ya Taifa.
d)     Kuaandaa vikao visivyopungua sita kwa mwaka kama kamati kuu.
e)      Kuandaa mikutano ya halmashauri kuu ya mkoa isiyo pungua miwili kwa mwaka.
f)       Kufanya ziara za mara kwa mara katika matawi na wilaya zao
g)      Kushiriki na kuhusika kwenye matukio ya mkoa na Taifa kwa ujumla
h)      Kuhudhuria na kushiriki vikao vya halmashauri kuu ya Mkoa na Taifa.
i)        Kujadili mwenendo mzima wa umoja na kupanga mikakati ya kuiendesha.
j)        Kupanga bajeti ya umoja na kuiwasilisha kwenye Halmashauri kuu.
k)       Kuibua na kupanga miradi mbalimbali ya umoja na kuijadili kwenye halmashauri kuu.
l)         Kupanga mipango ya muda mfupi na muda mrefu kwa ajili ya maendeleo ya umoja
m)    Kupitia maombi ya wanachama na kuyajibu na baadaye kuyawasilisha kwenye halmashauri kuu



Ibala13 :Kamati kuu ya Taifa
(i)                 Kamati kuu ya taifa inahusisha:-
Mratibu mkuu. Katibu mkuu. Mtunza hazina. Mwenykiti wa maombi. Makamu mwenyekiti wa maombi na mshauri wa Taifa.

(ii)               Wajibu wa kamati hii utakuwa:-
a)      Kusimamia shughuli zote za Taifa.
b)      Kuandaa agenda na kusimamia vikao vyote vya Taifa
c)      Kuandaa na kutoa taarifa zinazohusu shughuli zote za uendeshaji wa Taifa kwa halmashauri kuu ya Taifa.
d)     Kuaandaa vikao visivyopungua viwili kwa mwaka kama kamati kuu.
e)      Kuandaa mkutano wa halmashauri kuu ya Taifa kwa mwaka.
f)       Kufanya ziara za mara kwa mara  mikoani na wilaya inapobidi.
g)      Kushiriki na kuhusika kwenye matukio ya mikoa na Taifa.
h)      Kuhudhuria na kushiriki vikao vya halmashauri kuu ya Taifa na mikoa.
i)        Kujadili mwenendo mzima wa umoja na kupanga mikakati ya kuiendesha.
j)        Kupanga bajeti ya umoja na kuiwasilisha kwenye Halmashauri kuu.
k)       Kuibua na kupanga miradi mbalimbali ya umoja na kuijadili kwenye halmashauri kuu.
l)         Kupanga mipango ya muda mfupi na muda mrefu kwa ajili ya maendeleo ya umoja
m)    Kupitia maombi ya wanachama na kuyajibu na baadaye kuyawasilisha kwenye halmashauri kuu

Ibala 14:Halmashauri kuu.
(i)                 Halmashauri kuu inahusisha:-
Wajumbe wote wa umoja toka matawini (viongozi) na wawakilishi wawili walio teuliwa na  wachama wa ushirika kwa ngazi ya wilaya mkoa na Taifa.Na wanachama wote wa ushirika kwa ngazi ya Tawi.Washauri wakiwa ni wajumbe waalikwa.

(ii)               Wajibu wa halmashauri kuu.
a)      Mkutano Mkuu ndiyo kikao chenye madaraka ya juu ya uamuzi wa mwisho katika umoja 
b)       Kupokea taarifa za umoja kwa ngazi husika  na kuzipitisha au kuzijadili 
c)      Kuchagua viongozi wakuu wa umoja kwa ngazi husika.
d)     Kujadili mambo mbalimbali ya kuweza kuboresha umoja
e)       Kufanyia marekebisho katiba ya umoja kama ikibidi ili kuendana na mahitaji ya wakati
f)       Kupitisha bajeti na majina ya wanachama wapya




SEHEMU YA SABA
UCHAGUZI:
Ibala 15:Muda wa Uchaguzi.
(i)     Uchaguzi wa viongozi kwa ngazi zote utafanyika kila baada ya miaka miwili.
a)      Uchaguzi wa ngazi ya tawi utafanyika mwezi Februari na ngazi ya wilaya mwezi april
b)      Uchaguzi ngazi ya mkoa utafanika mwezi wa Juni na kwa ngazi ya Taifa utafanyika mwezi Disemba
c)      Watakao chaguliwa ni vijana wa kikristo wanaotoka katika madhebu ya kikristo na yanayotambulika kisheria na kijamii yenye ushuhuda mzuri na kukubarika.
.
(ii)   Muda wa kuongoza ni miaka miwili, kiongozi anaweza kuchaguliwa tena endapo atafanya kazi vema
Ibala 16:Kutambulisha Wagombea
(i)     Wagombea kwa ngazi ya tawi/wilaya watatambulishwa mara moja kabla ya uchaguzi
(ii)   Wagombea kwa ngazi ya mkoa na Taifa watatambulishwa mara tatu kwa wajumbe wa Halmashauri kuu kabla ya uchaguzi.
Ibala 17:Upigaji Kura.
(i)              Uchaguzi utakuwa ni wa siri
(ii)            Yatapendekezwa majina matatu (3) kwa kila kiti na kuungwa mkona za zaidi ya nusu ya wajumbe wa halmashauri kuu
(iii)          Atakayepata kura zaidi ya nusu atakuwa kiongozi
(iv)          Ikitokea kufungana kwa kura watarudia uchaguzi mara tatu na msimamizi atakuwa na kura ya uwamuzi
(v)            Mwanachama asie kuwa kijana wa kikristo, washauri na wachungaji hawatapiga kura.
Ibala 18:Viongozi waliochaguliwa.
(i)              Viongozi wapya waliochaguliwa watatangazwa na msimamizi wa uchaguzi kwa kusimamishwa na kutambulishwa mbele ya halmashauri kuu
(ii)            Watakabidhiwa uongozi na kimbukumbu za umoja na kusimikwa ndani ya siku tatu.
(iii)          Viongozi hawa watasimikwa na wachungaji/mchungaji atakaye alikwa kwaajili shughuli hii.




Ibala 19: MAPATO NA MATUMIZI.
a)      Mapato.
Ushirika utajipatia mapato kwa shughuli zilizo anzishwa na umoja ikiwa ni miradi pamoja na ada mbalimbali,kichango,sadaka,mikopo ubia na shughuli mbalimbali kutoka kwa wanachama.

b)      Matumizi ya fedha 
(i)     Kununua mali ghafi kwa ajili ya kazi za ushirika,
(ii)   Kuendesha matukio yote Muhimu ya ushirika huu ikiwa ni pamoja na kusaidia katika shughuli za umoja ambazo ni muhimu na zinahitaji fedha.
(iii) Kusaidia wahitaji pale inapotokea kwa makubalino ya wana uashika wa ngazi husika
(iv) Safari za kikazi za viongozi, watumishi au wawakilishi wa umoja kwenda kwenye matukio ya umoja na ya kijamii yatakayohusisha ushirika huu.
(v)   Kutoa michango na kulipa kodi mbalimbali
(vi)  

SEHEMU YA NANE
Ibala 20:HAKI ZA USHIRIKA WA VIJANA WA KIKRISTO TANZANIA
(i)     Ushirika wa vijana wa kikristo tanzania utakuwa na haki ya kushitaki au kushitakiwa kwa mujibu wa sheria za nchi. 
(ii)   Itakuwa na haki ya kubadili kifungu chochote cha katiba hii kwa Msajili wa Vyama /Vikundi yaani BASATA lazima ijulishwe mabadiliko ya katiba.
(iii)  utakuwa na haki ya kuhoji au kuratibu/kusimamia shughuli yoyote ya vijana wa kikristo itakayo endeshwa katika kila mkoa ikiwa na kwa vijana walio ndani ya umoja/ushirika huu.


 SEHEMU YA TISA
 Ibala 21: KUVUNJIKA/KUFA KWA USHIRIKA.
 Endapo kikundi itavunjika mambo yafuatayo yatafanyika. 
(i)     Itabidi kulipa madeni yote yanayodaiwa kama yapo kwa wakati. 
(ii)    Kudai mali au fedha zote zilizobaki kwa mtu binafsi/ Taasisi iliyokubaliana naye kabla 
(iii) Kugawana mali yote iliyobaki kwa usawa miongoni mwa Viongozi hai chini ya usimamini wa Viongozi wa Serikali Ya Mtaa. 
(iv) Madeni yote yatalipwa na umoja huu na yale ya kudai yatafuatiliwa na wadau wa umoja huu.


  9. MWISHO 
  Umoja huu sio mali ya mtu binafsi au maslahi ya mtu au watu wachache isipo kuwa ni kwaajili kristo na vijana wenye nia ya Kumtumikia Mungu.

UHALISIA WA MAISHA YA NDOA. SEHEMU YA KWANZA kabla hatuaja anagalia yaliyo katika ndoa Tutazame Maneno haya ya Daudi, Zaburi 127:1-2 &q...